• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 1:47 PM
KASHESHE: Walamba dili tamu

KASHESHE: Walamba dili tamu

Na THOMAS MATIKO

WANANDOA maceleb wakongwe, Nameless na Wahu wameangukia dili tamu ambayo itawaingizia fedha za kutosha, kisa mahusiano yao.

Nameless na Wahu wamedumu kwenye ndoa yao kwa miaka 15 sasa lakini mahusiano yao ya mapenzi ni zaidi ya miaka 20 toka walipoanza wakiwa Chuo Kikuu cha Nairobi.

Sasa wamelamba shavu ya kutengeneza filamu fupi (documentary) itakayosimulia maisha yao ya mapenzi na ndoa kwa miaka yote hiyo 15. Hii ni pamoja na walikoanzia, misukosuko ya penzi lao, muziki, skendo na matukio yote makubwa yaliyowahi kuwatokea kwenye ndoa yao.

Simulizi hiyo inayofahamika kama ‘This Love’ itakuwa na episodi 13. Episodi ya kwanza itapeperushwa Mei 2021 kwenye Showmax.

Filamu hii imetayarishwa na Young Rich inayomilikiwa na produsa Eugene Mbugua. Dili hiyo inadaiwa kuwa ya mamilioni kadhaa, pesa watakazopokea Nameless na mke wake.

You can share this post!

MATHEKA: Kanuni za kuzuia maambukizi ya corona shuleni...

DOMO KAYA: Mtakuja kupigwa kiboko!