• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 8:50 AM
Kenya yasitisha safari za ndege Somalia

Kenya yasitisha safari za ndege Somalia

Na MWANDISHI WETU

KENYA Jumatatu ilisitisha safari za ndege kwenda na kutoka Somalia kuashiria kuwa uhusiano kati ya mataifa hayo haujarejelewa ilivyotangazwa wiki jana.

Kulingana na notisi kutoka kwa Mamlaka ya Safari za Angani Kenya (KCAA) ndege za kuelekea au kutoka Somalia hazitahudumu kwa kipindi cha miezi mitatu, kuanzia jana.

Ni ndege zinazosafirisha misaada ya vyakula na dawa pekee ndio zitaruhusiwa nchini Kenya, mamlaka ya KCAA ilifafanua.

Asasi hiyo haikutoa sababu ya hatua hiyo lakini ikasema kumekuwa na agizo la kuiusalama kutoka serikali kwamba idhibiti usafiri wa anga kati ya nchini hizo mbili..

Uamuzi huo wa KCAA unamaanisha kuwa hata ndege za kukodiwa hazitaruhusiwa kusafiri hadi Somalia.

“Hata hivyo, ndege kutoka Somali, zinazopitia anga ya Kenya kuelekea mataifa mengine hazitaathiriwa na agizo hili,” itasema taarifa kutoka kwa mamlaka hiyo.

Vile vile, agizo hilo halitaathiri safari za ndege za kijeshi ambazo hazisimamiwi na mamlaka ya KCAA.

Tangazo hilo lilitokea wakati ambapo Rais wa Somalia Mohamed Farmaajo alikuwa akisafiri kupitia anga ya Kenya akiwa njiani kuelekea Uganda kuhudhuria hafla ya kuapishwa kwa Rais Yoweri Museveni.

Hatua hiyo, ya kuzimwa kwa safari za ndege kati ya Kenya na Somalia inaathiri juhudi za kurejesha uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili.

Wiki iliyopita Balozi maalum wa Qatari Mutlaq al-Qahtani aliingilia kwa nia ya kurejelewa kwa mahusiano ya kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili. Hii ni baada ya Somalia kukubali kufungua afisi yake ya kibalozi iliyofunga baada ya kukerwa na kile ilichotaja kama hatua ya Kenya kuingilia masuala yake ya ndani.

You can share this post!

Mvua yazua mafuriko na yaletea wakazi hasara

Waliong’aa KCSE wasimulia madhila waliyopitia