• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 4:31 PM
Ajabu ya shule moja kuandikisha ‘E’ kwenye masomo yote ya sayansi

Ajabu ya shule moja kuandikisha ‘E’ kwenye masomo yote ya sayansi

Na WYCLIFFE NYABERI

KARIBU watahiniwa wote walipata alama ya ‘E’ katika masomo ya sayansi kwenye shule moja Kaunti ya Kisii.

Watahiniwa 28 wa shule ya upili ya Rianyanchabera walipata alama ya E katika masomo ya Hisabati, Bayolojia na Kemia kwenye Mtihani wa Kidato cha Nne (KCSE) ambao matokeo yake yalitangazwa Jumatatu.

Ni watahiniwa wawili tu ambao walifanikiwa kupata alama ya D- kwenye masomo hayo.Watahiniwa wanne waliongoza katika shule hiyo, iliyoko katika eneobunge la Bomachoge Borabu, baada ya kupata wastani wa alama ya D.

Wengine 20 walifuatia kwa alama ya D- huku sita wakipata alama ya E. Katika eneobunge jirani la Nyaribari Chache, shule ya upili ya Boronyi haikuwa na sababu ya kusherekea.

Kati ya watahiniwa 22, tisa walipata alama ya D na 12 wengine wakaandikisha gredi za D-. Mwanafunzi mmoja aliandikisha alama ya E.Tulipotembelea shule hizo, makaribisho hayakuwa mazuri hata kidogo.

 

You can share this post!

CHARLES WASONGA: Elimu eneo la Kaskazini mwa Kenya...

Koome atofautiana na Maraga