• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
WINNIE ONYANDO: Wazazi watafute muda kuwajenga watoto wao kifikra na kimaadili

WINNIE ONYANDO: Wazazi watafute muda kuwajenga watoto wao kifikra na kimaadili

Na WINNIE ONYANDO

Kutafuta pesa si mbaya ila ujenzi wa ukuruba na ukaribu na mwanao ni wa maana zaidi. Uwepo wako kama mzazi katika maisha ya mwanao huchangia pakubwa katika ujenzi wa tabia na mienendo kwa mwanao. Pia huchangia pakubwa katika alama atakazozizoa mtoto akiwa shuleni.

Watoto wanapokua, mara nyingi wanahitaji umakini kamili kutoka kwa wavyele wake. Mama au baba anapokuwa mbali na mwanawe hasa anapokua na kumwona pengine mara mbili kwa wiki, basi uhusiano kati ya wawili hao huwa na umbali wa Mashariki na Magharibi.

Mzazi mama huwa mlezi na hivyo huwa karibu sana na mwanawe na kumpa muda mwingi sana ikilinganishwa na mzazi wa kiume ambaye mara nyingi hufunikwa na majukumu ya kuwakimu familia.

Ila ni jukumu la kila mzazi kumtengea mwanawe muda wa kuwa karibu naye, ahisi uwepo wake katika maisha yake. Kazi isiwe kikwazo kwa mzazi na kumtenga naye maishani. Afya ya mwanao ni bora kuliko pesa unazotafuta.

Kando na kuhitaji uwepo wako, mtoto anahitaji kujengwa kifikra, kuhakikishiwa kuwa ni mrembo au mtanashati kila mara, kupongezwa, kushughulikiwa kiafya na mengineyo.

Uwepo wako unampa mtoto motisha, ujasiri, nguvu, kumjenga kihisia, utulivu wa mawazo na fikra, furaha na amani ya kipekee moyoni.

Anapocheza au hata kutangamana na wenzake, anapata kuwasimulia jinsi anavyopendwa na wazazi wake. Jinsi yeye hupigwa pambaja, kuambiwa kuwa ni mtanashati au mrembo na kukumbatiwa na wazazi wake kabla ya kulala.

Mtoto huathiriwa mno na anachokiona au kushuhudia. Anapomwona babake anaishi na mamake kwa upendo na amani, yeye ataufuata mkondo huo na kuishi vivyo hivyo na mkewe.

Anapomwona ukimtesa na kumpiga mamake, naye ataishia kujua kuwa wanawake ni viumbe dhaifu wanaofaa kuchapwa kila mara.

Cha muhimu mno ni kumlea mwanao katika njia za Mungu. Mfunze kuwa watu hawafai kula bila kuomba, waongoze katika kuomba na kusoma Bibilia au Kuraan nyumbani kama mzazi.

Mfunze njia za Mungu maana Bibilia inasema kuwa ‘mlee mtoto katika njia ipasavyo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.’ Usifanye kazi au hata majukumu mengine yakutenganishe na mwanao.

Keti chini na mwanao, zungumza naye ili upate kufahamu mawazo, hofu, nguvu zake, udhaifu wake, talanta yake, rangi aipendayo, yanayompendeza na mahitaji zake za kibinafsi.

Usije ukajuta na kulalamika kuwa humfahamu mwanao ilhali wewe hukumtengea muda wa kumfahamu ipasavyo.Na WINNIE A ONYANDO

Wazazi wengi ‘wameolewa’ na kazi zao. Kutafuta pesa si mbaya ila ujenzi wa ukuruba na ukaribu na mwanao ni wa maana zaidi.

Uwepo wako kama mzazi katika maisha ya mwanao huchangia pakubwa katika ujenzi wa tabia na mienendo kwa mwanao. Pia huchangia pakubwa katika alama atakazozizoa mtoto akiwa shuleni.

Watoto wanapokua, mara nyingi wanahitaji umakini kamili kutoka kwa wavyele wake. Mama au baba anapokuwa mbali na mwanawe hasa anapokua na kumwona pengine mara mbili kwa wiki, basi uhusiano kati ya wawili hao huwa na umbali wa Mashariki na Magharibi.

Mzazi mama huwa mlezi na hivyo huwa karibu sana na mwanawe na kumpa muda mwingi sana ikilinganishwa na mzazi wa kiume ambaye mara nyingi hufunikwa na majukumu ya kuwakimu familia.

Ila ni jukumu la kila mzazi kumtengea mwanawe muda wa kuwa karibu naye, ahisi uwepo wake katika maisha yake.

Kazi isiwe kikwazo kwa mzazi na kumtenga naye maishani. Afya ya mwanao ni bora kuliko pesa unazotafuta.

Kando na kuhitaji uwepo wako, mtoto anahitaji kujengwa kifikra, kuhakikishiwa kuwa ni mrembo au mtanashati kila mara, kupongezwa, kushughulikiwa kiafya na mengineyo.

Uwepo wako unampa mtoto motisha, ujasiri, nguvu, kumjenga kihisia, utulivu wa mawazo na fikra, furaha na amani ya kipekee moyoni.

Anapocheza au hata kutangamana na wenzake, anapata kuwasimulia jinsi anavyopendwa na wazazi wake. Jinsi yeye hupigwa pambaja, kuambiwa kuwa ni mtanashati au mrembo na kukumbatiwa na wazazi wake kabla ya kulala.

Mtoto huathiriwa mno na anachokiona au kushuhudia. Anapomwona babake anaishi na mamake kwa upendo na amani, yeye ataufuata mkondo huo na kuishi vivyo hivyo na mkewe.

Anapomwona ukimtesa na kumpiga mamake, naye ataishia kujua kuwa wanawake ni viumbe dhaifu wanaofaa kuchapwa kila mara.

Cha muhimu mno ni kumlea mwanao katika njia za Mungu. Mfunze kuwa watu hawafai kula bila kuomba, waongoze katika kuomba na kusoma Bibilia au Kuraan nyumbani kama mzazi.

Mfunze njia za Mungu maana Bibilia inasema kuwa ‘mlee mtoto katika njia ipasavyo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.’ Usifanye kazi au hata majukumu mengine yakutenganishe na mwanao.

Keti chini na mwanao, zungumza naye ili upate kufahamu mawazo, hofu, nguvu zake, udhaifu wake, talanta yake, rangi aipendayo, yanayompendeza na mahitaji zake za kibinafsi.

Usije ukajuta na kulalamika kuwa humfahamu mwanao ilhali wewe hukumtengea muda wa kumfahamu ipasavyo.

You can share this post!

Beki Thiago Silva arefusha mkataba wake kambini mwa Chelsea...

AKILIMALI: Mwanamke aeleza biashara ya majeneza inavyompa...