• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Kaunti yatuma maafisa kuzima mzozo wa ardhi

Kaunti yatuma maafisa kuzima mzozo wa ardhi

Na CHARLES LWANGA

SERIKALI ya Kaunti ya Kilifi imetuma wataalamu kubainisha mpaka kati ya shamba la kunyunyuziwa maji la Galana-Kulalu na vipande vya ardhi vinavyomilikiwa na wenyeji ili kuzima uhasama.

Hii ni baada ya wakazi wa wadi ya Adu, eneobunge la Magarini kuandamana mapema wiki hii ripoti zilipoenea kuwa zaidi ya watu 20,000 watafurushwa ili kutoa nafasi ya upanuzi wa shamba hilo kubwa.

Waziri wa Ardhi Kaunti ya Kilifi, Bi Maureen Mwangovya, alithibithisha kuwa kumezuka mzozo wa ardhi baada ya jamii la eneo hilo na Shirika la Kustawisha Kilimo (ADC) kutofautiana kuhusu mipaka ya ardhi zao.

“Serikali ya kaunti ikishirikiana na serikali kuu tayari tumepeleka wataalamu wa ardhi eneo hilo la mzozo ili kufanya utafiti na kuleta ripoti itakayothibithisha mipaka ya eneo hilo,” alisema Mwangovya.

Wakiongozwa na Bw Jilo Onoto ambaye ni mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa jamii ya Watta, wakazi walilalamika kuwa serikali kupitia kwa ADC inaelekea kuwapokonya ardhi katika vijiji vya Mbaraka Jembe, Kaskini, Changoto, Kamale, Chamari, Chakama, Bombi.

Kando na kutegemea ardhi hizo kwa makao na kuchuma riziki mashambani, kuna pia majengo ya kijamii kama vile shule, misikiti, zahanati na misikiti ambayo wanahofia yatabomolewa.

You can share this post!

FWA yamtawaza beki Ruben Dias wa Manchester City Mchezaji...

Kaunti yasifu basari kwa kuboresha elimu