• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:23 PM
Kisumu ingali juu kwa visa vipya vya corona

Kisumu ingali juu kwa visa vipya vya corona

Na CHARLES WASONGA

KAUNTI ya Kisumu inaendelea kuongoza katika idadi ya visa vya maambukizi ya Covid-19 inayorekodiwa katika kila moja ya kaunti 47 nchini licha ya hakikisho la Gavana Anyang’ Nyong’o kwamba hali hiyo imedhibitiwa.

Kulingana na takwimu zilizotolewa na Wizara ya Afya Jumamosi, Kisumu ilinakili visa 103 vipya vya maambukizi ya virusi vya corona. Kaunti hii inafuatwa na Nairobi yenye visa vipya 61, Kitui (visa 57) huku Kericho ikirekodi visa vipya 43.

Hofu imeibuliwa kuhusu ongezeko la visa vya maambukizi ya corona Kisumu wakati ambapo inajiandaa kuwa mwenyeji wa Sherehe za Kitaifa za Sikukuu ya Madaraka mnamo Juni 1, 2021.

Mnamo Ijumaa ripotiz zilisema kuwa wadi za Covid-19 katika Hospitali Kuu ya Rufaa na Mafunzo ya Jaramogi Oginga Odinga zimejaa, kwa mara ya kwanza tangu mlipuko wa janga hilo uliporipotiwa nchini mwezi Machi 13, 2020.

Visa 103 vipya vilivyoripotiwa Kisumu ni sehemu ya jumla ya visa 573 vipya vilivyoripotiwa Jumamosi nchini Kenya baada ya sampuli 5,798 kupimwa.

You can share this post!

JAMVI: Mwamko mpya Pwani 2022

Barcelona wacharaza Eibar na kukamilisha kampeni za La Liga...