• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Muthama atoa masharti makali kabla ya kuridhiana na Kalonzo

Muthama atoa masharti makali kabla ya kuridhiana na Kalonzo

Na PIUS MAUNDU

MWENYEKITI wa chama cha UDA, Bw Johnston Muthama ameweka masharti makali kabla ya kushirikiana tena kisiasa na kinara wa Wiper, Kalonzo Musyoka.

Wawili hao walikosana miaka mitatu iliyopita, baada ya Bw Muthama kujiondoa katika kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha useneta wa Machakos mnamo 2017, na baadaye kuungana na kambi ya Naibu Rais Dkt William Ruto.

“Hatuwezi kushirikiana tena kisiasa hadi pale Bw Musyoka atajiondoa katika BBI pamoja na kuacha kuunga mkono handisheki kati ya Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga,” akasema Bw Muthama jana.Tofauti kati ya Bw Musyoka na Bw Muthama pia zimeenea kati ya viongozi wa Ukambani hasa kuhusiana na BBI.

Kati ya wale ambao wanapinga juhudi hizo ni Gavana wa Makueni Profesa Kivutha Kibwana na wabunge wanne wanaosema mabadiliko ya katiba hayafai kwa sasa, kwa kuwa kuna matatizo yanayopasa kushughulikiwa dharura.

Gavana wa Kitui Bi Charity Ngilu na mwenzake wa Machakos Dkt Alfred Mutua pia wanaunga mkono marekebisho ya katiba kupitia BBI ila wawili hao mara kwa mara wamekuwa wakikosana na Bw Musyoka hasa kuhusu siasa za uchaguzi mkuu wa 2022.

Maseneta Mutula Kilonzo Jnr (Makueni) na Enock Wambua wa Kitui pia wamekuwa wakionyesha msimamo wa uvuguvugu kuhusu BBI ili wasije wakakosoa siasa za Bw Musyoka.

You can share this post!

Hedhi salama bado ni changamoto kwa wasichana shuleni

Covid yalipuka Kisumu wiki baada ya ziara ya Uhuru, Raila