• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 11:05 AM
Chipu yapasua Mwamba raga ya kujiandalia Kombe la Afrika

Chipu yapasua Mwamba raga ya kujiandalia Kombe la Afrika

Na GEOFFREY ANENE

WANARAGA wa Chipu wamenyuka klabu ya Mwamba kutoka Ligi Kuu kwa alama 12-10 katika mechi ya kujipima nguvu uwanjani KCB Ruaraka mjini Nairobi, Jumamosi.

Chipu, ambao wanajiandaa kutetea taji la Kombe la Bara Afrika kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 (Barthes Trophy), walifunga miguso miwili na mkwaju mmoja nao mabingwa wa ligi 1983 Mwamba walipata miguso miwili bila mkwaju.

Vijana wa kocha Curtis Olago ni wenyeji wa Barthes Cup kutoka Juni 26 hadi Julai 3 ugani Nyayo.Wameratibiwa kupepetana na Senegal mnamo Juni 26, Madagascar (Juni 29) na miamba Namibia (Julai 3).

Haijabainika wazi kama Namibia itashiriki. Vyombo vya habari nchini humo vilisema Juni 4 kuwa imejiondoa kwa sababu ya marufuku dhidi ya michezo ya kugusana kutokana na ongezeko la maambukizi ya virusi vya corona nchini Namibia.

Kambi ya Chipu inasema haijapata habari za Namibia kujiondoa. Chipu ilitawazwa bingwa wa mwaka 2019 baada ya kuduwaza Namibia 21-18 katika fainali ugani KCB Ruaraka.

 

  • Tags

You can share this post!

Vihiga Queens na Thika Queens walishinda zoni zao za Ligi...

36 kuhojiwa kujaza nafasi 4 za makamishna IEBC