• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 7:55 PM
Spika Muturi awarai madaktari watumie teknolojia kwa tiba

Spika Muturi awarai madaktari watumie teknolojia kwa tiba

Na Ruth Mbula

SPIKA wa Bunge la Kitaifa, Bw Justin Muturi, amewarai wadau wa afya kuharakisha utekelezaji wa taratibu za kutumia teknolojia kutoa huduma za afya katika hospitali za humu nchini.

Bw Muturi alisema hospitali zinapaswa kukumbatia mfumo huo wa kisasa hususan wakati huu nchi inakabiliwa na janga la corona, kama njia ya kutimiza malengo ya kitaifa ya kutoa Afya kwa Wote (UHC).

Haya yanajiri huku wizara za Afya na Habari, Mawasiliano na Teknolojia (ICT) zikitangaza kuwa zinaendesha mikakati kushinikiza matumizi ya teknolojia katika sekta ya afya nchini. Wadau wanahoji hilo litapunguza mno maambukizi ya corona.

Bw Muturi alikuwa akizungumza Jumamosi alipofunga kongamano la sayansi la kila mwaka, la Chama cha Kitaifa cha Madaktari (KMA).

Kongamano hilo la siku tatu lilifanyika katika hoteli moja Kaunti ya Kisii na kuhudhuriwa na madaktari kutoka sehemu mbalimbali nchini.

Bw Muturi alisema kuwa Afya kwa Wote (UHC) ni mojawapo ya malengo makuu ya serikali yaliyo kwenye Ajenda Nne Kuu za Maendeleo.

“Kutokana na idadi ndogo ya madaktari tuliyo nayo nchini, hatutaruhusu hali ambapo madaktari wetu wataendelea kuhamia katika nchi nyingine. Ni wakati tukumbatie matumizi ya teknolojia katika sekta hii ili kuboresha huduma tunazotoa,” akasema.

You can share this post!

Mjukuu wa Moi asusia DNA, hatarini kushtakiwa

Mvulana aliyeitwa shule ya wasichana sasa apata afueni