• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Mvulana aliyeitwa shule ya wasichana sasa apata afueni

Mvulana aliyeitwa shule ya wasichana sasa apata afueni

Na Francis Mureithi

WAZIRI wa Elimu, Prof George Magoha, amekubali lawama ambapo mwanafunzi mvulana katika Kaunti ya Bungoma aliitwa shule ya upili ya wasichana kujiunga na kidato cha kwanza.

Spencer Wangila kutoka Bungoma alipokea barua ya kujiunga na Shule ya Upili ya Wasichana ya Naromoru, Kaunti ya Nyeri.

Ni hali iliyoacha familia ya mvulana huyo katika hali ya kuchanganyikiwa, kwani kijana wao hakuchagua shule ya Naromoru kuwa miongoni mwa zile ambazo angependa kujiunga nazo.

Wangila alifanya Mtihani wa Darasa la Nane (KCPE) katika Shule ya Msingi ya Misikhu, na kuzoa alama 370.

Lakini akizungumza Ijumaa katika hafla ya kufuzu kwa mahafala wa Chuo Kikuu cha Egerton, Prof Magoha alihakikishia familia hiyo kuwa tatizo hilo limerekebishwa.

“Kama Waziri wa Elimu, ninakubali lawama zote kutokana na kosa hilo. Hata hivyo, ningetaka kuwahakikishia wananchi na wazazi wa mwanafunzi husika kuwa kosa hilo limerekebishwa.

Ni makosa kuwa mvulana huyo aliitwa katika shule ya wasichana japo nina furaha kwani hali hiyo haipo tena,” akasema.

Akaongeza: “Mwanafunzi huyo sasa ameitwa katika Shule ya Upili ya Kibabi, ambayo ni ya wavulana.”

You can share this post!

Spika Muturi awarai madaktari watumie teknolojia kwa tiba

Viongozi walalamikia Rais kutojali Mlima Kenya