Na MARGARET MAINA
ILI uwe na ngozi nzuri yenye kuvutia, unahitaji uvumilivu na uratibu wa mpangilio fulani.
Si swala la siku moja.
Huu hapa ni utaratibu wa kukuelekeza ili uwe na ngozi inayovutia.
Maji
Anza siku yako kwa glasi ya maji fufutende yenye slesi kadhaa ya limau ndani yake.
Hakikisha unakunywa si chini ya glesi nne za maji kwa siku.
Maji husaidia ngozi kuwa na afya na yenye kuvutia.
Unywaji maji ya kutosha unafanya ngozi yako iwe na rutuba na kuondoa mikunjo.
Kujipenda
Unachojisikia ndani ya moyo wako ndicho ambacho kitatoka nje. Ukiwa na msongo wa mawazo kwa kujijadili kuhusu mwonekano wako, kuna uwezekano kwamba ngozi yako itaharibika. Hakikisha unajisifu kila siku kwa kuwa na mawazo chanya zaidi maishani.
Utunzaji wa ngozi
Unahitaji kuijali ngozi yako kwa kununua vipodozi vinavyoendana na ngozi yako. Pia kula vyakula vinavyorutubisha ngozi yako. Vile vile ni muhimu upake sun screen kuikinga ngozi dhidi ya miale hatari ya jua na kuwa na mpangilio wa kuitunza ngozi yako.
Usingizi wa kutosha
Hakikisha unalala kwa muda wa saa nane (8) si chini ya mara nne kwa wiki.
Faida za kupata usingizi wa kutosha