• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 8:27 PM
Afisa Mkuu Mtendaji wa AC Milan, Ivan Gazidis, augua saratani ya koo

Afisa Mkuu Mtendaji wa AC Milan, Ivan Gazidis, augua saratani ya koo

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

AC Milan wamethibitisha kwamba Afisa Mkuu Mtendaji wa kikosi chao, Ivan Gazidis, amepatikana na saratani ya koo.

Miamba hao wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A) wameshikilia kwamba wanatarajia Gazidis, 56, kupona haraka iwezekanavyo baada ya kuanza matibabu.Gazidis alihudumu kambini mwa Arsenal kwa kipindi cha miaka 10 kabla ya kuhamia AC Milan mnamo 2018.

Kwa mujibu wa AC Milan, kinara huyo bado atasalia ofisini kutekeleza majukumu yake wakati atakapokuwa akiendelea na matibabu.

 

  • Tags

You can share this post!

Arsenal wajiondoa kwenye Florida Cup baada ya kikosi...

Familia 100 zilizopoteza nyumba zao katika kisa cha moto...