Na MASHIRIKA
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO
AC Milan wamethibitisha kwamba Afisa Mkuu Mtendaji wa kikosi chao, Ivan Gazidis, amepatikana na saratani ya koo.
Miamba hao wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A) wameshikilia kwamba wanatarajia Gazidis, 56, kupona haraka iwezekanavyo baada ya kuanza matibabu.Gazidis alihudumu kambini mwa Arsenal kwa kipindi cha miaka 10 kabla ya kuhamia AC Milan mnamo 2018.
Kwa mujibu wa AC Milan, kinara huyo bado atasalia ofisini kutekeleza majukumu yake wakati atakapokuwa akiendelea na matibabu.