• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:58 PM
Poghisio ataka Lonyangapuo kuhama Kanu

Poghisio ataka Lonyangapuo kuhama Kanu

Na OSCAR KAKAI

KIONGOZI wa Wengi katika Seneti, Samuel Poghisio amemtaka Gavana wa Pokot Magharibi, John Lonyangapuo kuhama Kanu na kutafuta chama kipya.

Prof Lonyangapuo ndiye gavana pekee aliyechaguliwa kwa tiketi ya Kanu.

Wito wa Bw Poghisio umechochea vita vya maneno kati ya viongozi hao wawili ambao walifanya kampeni pamoja na kuchaguliwa kwa tiketi ya Kanu mnamo 2017, lakini wakatofautiana mwaka jana.

Wiki iliyopita, Prof Lonyangapuo alitangaza kwamba ameondoka Kanu na atawania kwa tiketi tofauti 2022.

Alisema hivi karibuni, yeye pamoja na aliyekuwa gavana wa Pokot Magharibi Simon Kachapin, Naibu Gavana wa Pokot Magharibi Nicholas Atudonyang, Spika wa Bunge la Kaunti hiyo Catherine Mukenyang, miongoni mwa viongozi wengine, watamtaja mmoja wao atakayemenyana na Bw Lonyangapuo katika uchaguzi wa 2022.

“Huwezi kung’atuka chamani bila kufuata sheria. Prof Lonyangapuo bado ni mwanachama wa Kanu,” alisema Bw Poghisio.

You can share this post!

Sitishiki hata ukinitimua Wiper, Kibwana aambia Kalonzo

Vigogo wawania Mlima Kenya kama mpira wa kona