• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 11:55 AM
Rais awaongoza Wakenya kumwomboleza mumewe waziri Amina Mohamed

Rais awaongoza Wakenya kumwomboleza mumewe waziri Amina Mohamed

Na WINNIE ONYANDO

RAIS Uhuru Kenyatta anawaongoza Wakenya katika kutoa rambirambi kwa Waziri wa Michezo na Turathi Bi Amina Mohamed kufuatia kifo cha mumewe Bw Khalid Hossain Ahmed.

Familia ya mwendazake wamethibitisha kifo cha mfanyabiashara huyo mashuhuri ambaye ameaga dunia Alhamisi asubuhi katika hospitali ya Nairobi baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Rais amemtaja kama mfanyabiashara mpole na mwenye bidii katika mambo yake.

“Tumempoteza mwanamume kidete na mpenda familia yake. Bw Ahmed amechangia sana katika shughuli za kuinua uchumi nchini,” aliomboleza Rais Kenyatta.

Japo Bi Amina anafahamika nchini, wawili hao hawakuanika sana maisha yao ya ndoa kwa umma.

Mnamo Machi 2021 Bi Amina alimpoteza ndugu yake, Bw Esmael Mohammed Jibril ambaye pia alikuwa mfanyabiashara tajika nchini.

You can share this post!

Malkia Strikers yapigwa na Serbia kwenye Kundi A voliboli...

Kinara wa mashindano ya baiskeli nchini Ujerumani afurushwa...