• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 PM
Pochettino matumaini juu PSG ikigaragazana na Lille katika Kombe la Tel Aviv

Pochettino matumaini juu PSG ikigaragazana na Lille katika Kombe la Tel Aviv

Na MASHIRIKA

KOCHA Mauricio Pochettino ameweka matumaini juu kwa klabu yake Paris Saint German, washindi wa French Cup wakisubiri kuchuana na washindi wa ligi katika kipute cha Tel Aviv French Champions Trophy.

Pochettino aliwataka wachezaji wake kucheza kwa nia ya kushinda bali sio kulipiza kisasi dhidi ya timu yoyote ile.

Pochettino anaanza msimu mpya wa kwanza baada ya kutwaa mikoba ya timu hii kutoka kwa Thomas Tuchel, aliyepigwa kalamu katikakati ya msimu jana.

PSG wataikabili Lille bila huduma za Neymar, ambaye bado ako Brazil na sajili wapya; Mhispania Sergio Ramos na mlindalango Mwitaliano Gianluigi Donnarumma.

Kikosi hicho kitafaidi huduma za wachezaji matata Kyllian Mbappe, Marco Verrati na Angel Di Mria ambao wako tayari kwa ngarambe hiyo.

Kocha huyu amesisitiza nia yake ya kupigania mataji yote muhimu, huku akiahidi kuijenga timu hiyo kuboreka zaidi baada ya msimu jana kwenda kombo.

“Kupoteza ligi kuu, kubanduliwa katika Nusu-Fainali za Champions League kulituacha na hisia kali,” alisema.

Lille walipiga breki ubabe wa PSG misimu mitatu mfululizo, wakiwapiku kwa pointi moja muhimu. Lille walitamatisha msimu kwa alama 83, PSG wakifuatia kwa alama 82.

PSG na Lille wataanza msimu mpya dhidi ya Troyes na Metz mtawalia, wote wakisakatia mechi zao ugenini.

TAFSIRI NA: NDUNGI MAINGI

You can share this post!

Kenya yasajili visa vipya 1,259 vya Covid-19 kufikisha...

MUTUA: Chocheo la vita Ethiopia ni ukabila, manyanyaso