• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Kamishna aagiza wauzaji wa barakoa feki wanaswe

Kamishna aagiza wauzaji wa barakoa feki wanaswe

Na TOM MATOKE

MAAFISA wa Usalama katika Kaunti ya Nandi wameagizwa kukamata wafanyabiashara wanaouza barakoa feki.

Kamishna wa Kaunti ya Nandi Herman Shambi, alisema kuwa barakoa nyingi zinazouzwa kwa kati ya Sh5 na Sh10 katika miji mbalimbali ya Kaunti hiyo ni feki na zinachangia kusambaa kwa virusi vya corona.

Alisema kuwa maelfu ya wafanyabiashara wamefurika katika miji mbalimbali ya kaunti hiyo kuuza barakoa hizo zisizo na uwezo wa kuzuia virusi.

“Ndani ya miezi mitatu iliyopita, Kaunti ya Nandi imepoteza watu 54 kutokana na virusi vya corona. Nandi inapakana jimbo moja na kaunti za Nyanza na Magharibi ambazo zina maambukizi ya juu ya virusi vya corona,” akasema Bw Shambi.

Kamishna huyo pia alisema kuwa maafisa wa usalama watakamata watu watakaopatikana wakila chakula matangani na sherehe za harusi.

Aliagiza kuwa miili ya watu wanaofariki izikwe ndani ya saa 72 na machifu watekeleze marufuku ya waombolezaji kula matangani.

Bw Shambi pia aliagiza machifu kuhakikisha kuwa idadi ya waombolezaji wakati wa mazishi haipiti watu 50.

Bw Shambi aliyeandamana na Naibu Gavana wa Nandi Dkt Yulita Mitei na waziri wa afya Ruth Koech, alikuwa akizungumza alipoongoza kamati ya kukabiliana na corona mjini Kapsabet.

Aliagiza wahudumu wa matatu kuhakikisha kuwa abiria wote wanavalia barakoa.Naye Bw Koech alifichua hospitali za kaunti hiyo hazina gesi ya oksijeni ya kutosha.

 

You can share this post!

Kalonzo amrai Shahbal arejee chamani Wiper

Wazozana kuhusu ufanikishaji miradi