• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Juhudi za Naibu Rais kupenya Ukambani zapata pigo kubwa

Juhudi za Naibu Rais kupenya Ukambani zapata pigo kubwa

Na PIUS MAUNDU

JUHUDI za Naibu Rais William Ruto kupenya katika Kaunti ya Kitui ziligonga mwamba baada ya madiwani 15 waliokutana naye wiki hii kubanduliwa katika kamati za bunge la kaunti.

Spika wa bunge la Kaunti ya Kitui, George Ndotto aliwasuta madiwani hao walioandamana na aliyekuwa naibu gavana wa Nairobi, Jonathan Mueke kukutana na Dkt Ruto katika makazi yake rasmi mtaani Karen, Nairobi.

“Tunatenga Bunge la Kaunti ya Kitui na vitendo vya madiwani waliokutana na Dkt Ruto,” Bw Ndoto alisema kwenye taarifa na kuongeza kuwa Naibu Rais hatapenya katika ngome hiyo ya kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka.

“Tunataka ifahamike kwamba sisi wawakilishi wa Kaunti ya Kitui tuko nyuma ya mgombea urais wetu Stephen Kalonzo Musyoka kwenye uchaguzi mkuu wa 2022. Hakuna kitakachotufanya tubadilishe msimamo wetu. Tunataka Wakenya wajue kuwa Kalonzo Musyoka anaungwa mkono kikamilifu katika kaunti yake ya nyumbani na tunawahimiza wampe heshima anayohitaji kuongoza nchi hii.”

You can share this post!

Mshirika wa Ruto ni mhalifu, asema waziri Matiang’i

Vifaranga wapya wa Raila