• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 3:23 PM
Corona ilivyohangaisha makahaba dhuluma zikiongezeka

Corona ilivyohangaisha makahaba dhuluma zikiongezeka

NA RICHARD MAOSI

MAKAHABA kutoka Magharibi mwa Kenya wamekuwa wakipitia hali ngumu ya kiuchumi tangu janga la corona kubisha humu nchini.

Wanasema wamekuwa wakipitia masaibu chungu nzima, baadhi yao wakibakwa, kuuawa na wengine kunyanyaswa kijinsia katika harakati ya kila kitu kutafuta riziki.

Muungano wa Makahaba wa Magharibi Western Sex Workers Association(Wekeswa) kupitia mratibu wao wa eneo la Magharibi J.O, wamekuwa windo rahisi kwa wateja wanaodai ngono cha nguvu na maafisa wa usalama.

Alieleza kuwa wamekuwa wakihangaishwa na wateja katika maeneo ambayo walidhani ni salama.

“Ni hali ambayo imekuwa ikileta unyanyapaa kwa kuhisi kubaguliwa katika sehemu ambazo awali tulikuwa tukiendesha biashara bila woga wa kupotea maisha,”J.O akasema.

Anasema kuwa mnamo 2020 waliamua kuchukua hatua isiyokuwa ya kawaida kujikinga.

Aidha alieleza kuwa Wekeswa ni muungano wa zaidi ya makundi 11 kutoka Kisumu, Migori, Homabay, Mumias, Siaya , Bungoma na kwingineko.

“Matatizo yalianza wakati ambapo wateja wengi walipoteza kazi serikali ikiwaomba kujikinga dhidi ya msambao wa covid-19, waliposhauriwa kuchukua tahadhari za kukaa nyumbani na kudumisha umbali wa mita moja,”akasema.

J.O aliongezea kuwa wengine wao walilazimika kurejea mashambani waliposhindwa kulipa hata kodi za nyumba.

“Walioshindwa kustahili shinikizo la kupata hela waligeukia ulevi, wakitumai kuwa wangefanikiwa kutuliza mawazo, ndio maana tuliamua kusaka msaada wa kitaaluma kuwasaidia wenzetu kujinasua kutoka kwa kwa matatizo kama haya,”

Aidha alisuta baadhi ya vyombo vya habari kwa kufanya mahojiano na wanachama wao bila kupata idhini kutoka kwa muungano wa Wekeswa, jambo ambalo limekuwa likiwaharibia jina kwa umma.

J.O alisema kuwa baadhi ya wanachama kutoka Magharibi na Nyanza wamekuwa wakitafuta tenda kutoka kwa serikali, ila hawana uwezo kutokaa na kipato cha chini.

Aidha vyumba vya burudani ambapo wamekuwa wakiendesha biashara yao vilifugwa makali ya Covid-19 yalipoendelea kusambaa nchini.

Aliongezea kuwa licha ya changamoto nyingi wamefanikiwa kusomesha ndugu zao mpaka kiwango cha Chuo Kikuu kutokana na hela za ukahaba.

“Nilipokuwa darasa la saba nilipoteza wazazi wangu wote, jamaa zangu walinyakua urithi ingawa nilifanikiwa kufika kidato cha nne, hivi sasa ninapigania haki za makahaba wenzangu katika eneo la Magharibi,”alisema.

J.O aliongezea kuwa katika mtaa wa Nyalenda kuna zaidi ya makahaba 300, wengi wao wakiwa ni wanafunzi walioingilia biashara hii wakati wa likizo ndefu ya 2020.

Wengi wamekuwa wakipata ujauzito, na kuanza kuwategemea marafiki zao wawasaidie kulisha watoto wao.

J.O analenga kuwasaidia wasichana kama hawa akiamini kuwa watarejea shuleni, na watafanikiwa kupata walezi ambao watawasaidia kulinda watoto.

“Kabla ya Covid-19 kuingia nchini tulikuwa na makahaba 5000 pekee mjini Kisumu lakini hivi sasa wamefikia 7000 na idadi yao inaendelea kuongezeka hususan sehemu za mijini,”

Hata hivyo kaunti ya Bungoma na Trans Nzoia zimekuwa na idadi ndogo ya wanawake ambao wanaendesha biashara ya ngono.

Msemaji wa Wekeswa P.O aliomba vyombo vya habari kukoma kuwaharibia jina makahaba kwani ni wafanyikazi kama mawakili, tabibu na walimu.

Vilevile alieleza kuwa wameweka mpangilia kabambe wa kustaafu hususan kwa wale ambao wamejiendeleza kimaisha kwa kuongeza kiwango cha elimu.

Alisema kuwa wa punde zaidi kuachana na kazi ya ukahaba meendea taaluma ya utabibu, wengine 30 walifaidika Sh 1000 za kila siku za Covid Relief Fund, huku wengine 40 wakipata nafasi katika mradi wa Kazi Mitaani.

You can share this post!

Wafuasi wa Ruto wamtongoza Kingi ajiunge na...

Polisi sita wanaohusishwa na mauaji ya ndugu wawilli wa...