• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 6:27 PM
Wafungwa waachiliwa kupunguza msongamano

Wafungwa waachiliwa kupunguza msongamano

Na Manase Otsialo

Wafungwa 18 wameachiliwa huru kaunti ya Mandera baada ya hukumu zao kuchunguzwa na Kamati ya Taifa ya Huduma ya Jamii.

Kuachiliwa kwao kunafuatia hatua za kupunguza idadi ya wafungwa magerezani ili kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona.

Katika Kaunti ya Mandera, idara ya probesheni ya iliwasilisha majina ya wafungwa 36 katika juhudi za kupunguza msongamano katika magereza.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Garissa, Abida Aaron aliachilia tisa mara moja na kuweka watatu katika probesheni.

Aliagiza saba washiriki kazi ya jamii na mmoja akapunguziwa kifungo kutoka miaka mitano hadi mitatu.

Mahakama Kuu ilikataa pendekezo la kuchunguza vifungo vya wafungw wanane.Wakati wa uchunguzi huo, maafisa wa probesheni huwa wanazingatia muda ambao mfungwa ametumikia, tabia yake akiwa gerezani, aina ya makosa aliyotenda na maoni kutoka kwa waathiriwa na jamii.

Wafungwa wa makosa ya kujaribu kuua, uchomaji mali, ulanguzi wa binadamu na watoto na mengine makubwa hawashirikishwi kwenye mpango wa kupunguza msongamano katika magereza.

Baada ya kuachiliwa huru, huwa wanawekwa chini ya usimamizi wa maafisa wa probesheni.

You can share this post!

Ogiek, Ndorobo waomba kikao na Rais kuhusu ardhi

Chama cha Kiswahili shuleni Kitengela International ni...