Na TITUS OMINDE
VIJANA 15 wa kurandaranda mjini Eldoret, walikiri mashtaka ya kukosa kuvalia barakoa. Vijana hao walipatikana katika maeneo tofauti ya umma mjini Eldoret.
Hata hivyo, korti iliwaachilia huru baada ya kuwaonya dhidi ya kukosa kuvalia barakoa.Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Eldoret, Bw Barnabas Kiptoo, alielezwa kuwa washukiwa walikamatwa wakati wa msako wa wato wanaokiuka kanuni za kudhibiti msambao wa corona.
“Hata kama mahakama hii imewasamehe kwa onyo kwamba ikiwa utarudia kosa lile lile utakamatwa, kuvaa barakoa ni kwa afya yako na watu walio karibu nawe, si adhabu,” hakimu aliwaeleza.