• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Waiguru ateuliwa kati ya wanawake 100 bora bara Afrika

Waiguru ateuliwa kati ya wanawake 100 bora bara Afrika

Na KENYA NEWS AGENCY

GAVANA wa Kirinyaga, Jumatatu aliteuliwa na Kituo cha Habari cha Avance kati ya wanawake 100 bora wenye ushawishi mkubwa Afrika.

Bi Anne Waiguru aliteuliwa pamoja na viongozi mbalimbali Afrika ambao wamekuwa na ushawishi na mafanikio makubwa kwa umma.

Kampuni ya Avance inahusika na kubadilisha simulizi kuhusu Waafrika kupitia ukadiriaji na viwango vya ushawishi kwa umma. Nia ya uteuzi huo ni kuonyesha na kusherehekea mafanikio ya wanawake 100 bora barani Afrika.

Uteuzi huo unajumuisha uongozi bora, utendakazi, mafanikio ya kibinafsi na uwezo wa kushawishi jamii.

Miongoni mwa viongozi walioteuliwa ni aliyekuwa rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, rais wa Ethiopia, Sahle-Work Zedwe, rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, rais wa Ligi ya Wanademokrasia wa Kongo, Angele Makombo, aliyekuwa naibu rais wa Gambia, Aja Fatouma Tambjang, katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Amina J Mohamed, jaji mkuu, Martha Koome na gavana wa Kitui, Charity Ngilu.

Kituo hicho cha Avance kilisema walioteuliwa watatoa mafunzo kwa wanawake viongozi kupitia programu ya ‘Be a Girl’.

Mnamo 2017, Bi Waiguru alichaguliwa kati ya magavana watatu wa kwanza wanawake nchini.

Baadaye mwaka huo huo, alichaguliwa kama Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Magavana na pia kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kushika wadhifa huo.

You can share this post!

Matumaini kiwanda kikipokea Sh30m

Vihiga Queens kufufua uadui na CBE ya Ethiopia kwenye...