• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:55 AM
Museveni akemea mapinduzi Guinea

Museveni akemea mapinduzi Guinea

Na AFP

KAMPALA, UGANDA

RAIS wa Uganda Yoweri Museveni ametoa wito kwa wanajeshi wa Guinea waliofanya mapinduzi dhidi ya serikali mapema wiki hii wajiondoe serikalini kwa kuwa wanalirejesha taifa hilo nyuma.

Kiongozi huyo alikemea mapinduzi hayo, aliyosema hayakufaa na inaonyesha tu tamaa ya wanajeshi ya kutawala Guinea.

“Waliotekeleza mapinduzi hayo wanafaa wajiondoe kwa sababu wao ni sehemu ya matatizo yanayozonga nchi hiyo. Mapinduzi yamekuwa yakifanyika tangu miaka ya 60 na yamechangia changamoto mbalimbali zinazolikumba bara la Afrika. Nawakemea wote waliohusika,” akasema Rais Museveni.

Rais wa Guinea Alpha Conde ambaye ameongoza taifa hilo kwa mihula mitatu aliondolewa mamlakani mnamo Jumapili na wanajeshi kutoka kitengo spesheli cha kijeshi.

Kiongozi huyo alilaumiwa kwa kushiriki ufisadi na kutumia vibaya fedha za umma.

Ingawa hivyo, raia wengi wa Guinea wamekemea mapinduzi hayo na kusisitiza kuwa wanaunga mkono Rais Conde ambaye ana umri wa miaka 83.

Rais Museveni pia alisema kuwa uamuzi wake wa kuwakubali wakimbizi kutoka Afghanistan ulitokana na kuguswa na madhila waliokuwa wakiyapitia baada ya kundi la Taliban kuchukua usukani.

You can share this post!

Wanawake wataka Taliban iwape vyeo

Muturi adai uhasama umeathiri Bunge