Na MARGARET MAINA
ULAJI wa chakula unaofaa ni ule ambao mtu anahakikisha kwamba anakila chakula mchanganyiko, cha kutosha na chenye virutubisho vyote kwa uwiano unaotakiwa.
BNi muhimu mtu ale matunda angalau mara mbili kwa siku na ale mboga kwa wingi.
Ni muhimu kuhakikisha unatumia mafuta kwa kiasi kidogo. Mafuta ya nyama sio mazuri sana kwani yanahusishwa na magonjwa ya moyo. Badala yake inashauriwa mtu atumie zaidi mafuta yatokanayo na mimea.
Matumizi ya sukari na chumvi yawe ya kiasi. Pia kwa watu wanaokunywa pombe wasinywe kupita kiasi.
Kula chakula mchanganyiko
Chakula mchanganyiko hukuwezesha kupata virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini. Kwa mfano vyakula vya wanga vinasaidia kuupa mwili nguvu na joto. Protini hutumika kujenga mwili navyo vitamini na madini hulinda mwili dhidi ya magonjwa. Kila siku jitahidi kula vyakula kutoka katika makundi yafuatatyo:
Epuka mafuta mengi
Mafuta mengi mwilini hasa yale yenye asili ya wanyama yanaweza kusababisha ongezeko la magonjwa ya moyo na shinikizo kubwa la damu,. Hivyo inashauriwa kutumia zaidi mafuta yatokanayo na mimea.
Jinsi ya kupunguza mafuta
Kula matunda na mbogamboga kwa wingi
Vyakula hivi huupatia mwili kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali kama vile baadhi ya magonjwa ya moyo, saratani na kisukari.
Matunda ni chanzo cha virutubisho kama vile vitamini na madini ambayo hupatikana kwa wingi kwenye vyakula hivi kuliko kwenye vyakula vingine. Virutubisho hivi:
Virutubisho hivi havihifadhiki katika mwili wa binadamu hivyo ni vizuri matunda tofauti yajumlishwe kwenye mlo/milo ya siku.
Inashauriwa ifuatavyo kuhusu matunda na mbogamboga
Vyakula vyenye nyuzinyuzi
Vyakula vyenye nyuzinyuzi (fibre) husaidia katika usagaji wa chakula tumboni na pia huweza kupunguza baadhi ya aina za saratani, magonjwa ya moyo na kisukari. Ili kuongeza nyuzinyuzi:
Punguza chumvi
Punguza sukari
Sukari huongeza nishati mwilini, hivyo huchangia kuongezeka kwa uzito. Matumizi ya sukari huzalisha bakteria kinywani ambao husababisha meno kutoboka. Hivyo inashauriwa: