Na MARGARET MAINA
Fanya mazoezi
Zoezi ni jambo lolote linalohusisha misuli na kusababisha kuongezeka kwa mapigo ya moyo na kupumua kwa kasi. Kiwango kinacholeta faida ni mazoezi yasiyopungua dakika 30 kwa siku angalau siku tano kwa wiki.
Faida za mazoezi na kujishughulisha ni:
Mifano ya kujishughulisha
Kwa wale wenye kazi za kukaa, ni vyema kufuatilia shughuli kwa kutembea kuliko kutumia teknolojia kama kupiga simu kwa mtu uliye naye katika jengo moja, kufuatilia mwenyewe badala ya kutumana na kadhalika.
Mazoezi ni pamoja na kutembea, kukimbia, kuruka kamba, na kuendesha baiskeli. Anza taratibu, fanya mazoezi kwa dakika 20 – 30 na fanya angalau mara 3 – 4 kwa wiki.
Epuka msongo wa mawazo
Kuwa na mawazo mengi kunaweza kukuletea mfadhaiko na magonjwa kama vile kuumwa na kichwa au shinikizo la damu, kukosa usingizi, kukosa hamu ya chakula au unywaji wa pombe kuzidi kipimo. Mambo ya kufanya unapojisikia una uchovu na msongo wa mawazo:
Kutotumia tumbaku
Tumbaku inaweza kutumika kwa kuvuta kama vile sigara/msokoto/kiko, kunusa na kutafuna. Utumiaji wa tumbaku unahusishwa sana na saratani ya mapafu, vidonda vya tumbo, kifua sugu na magonjwa mengine mengi.
Athari za utumiaji tumbaku katika viungo mbalimbali vya mwili
Punguza unywaji wa pombe
Utumiaji mbaya wa pombe kwa kiasi kikubwa husababisha madhara makubwa kiafya hivyo ni vyema kwa watumiaji wa pombe kunywa pombe kiasi au kuacha kabisa jinsi zinavyoshauri dini mbalimbali.
Madhara yatokanayo na matumizi mabaya ya pombe
Faida zitokanazo na kutotumia pombe vibaya
Kutotumia au kunywa tu kwa kiasi kuna faida zifuatazo:
Mwili wa binadamu haukuumbwa ili kuhifadhi mafuta mengi. Hali ya uzani kupita kiasi na kitambi inahusishwa na madhara mbalimbali ya kiafya.