• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
Kinara wa chama cha UGM, Neto aitaka IEBC isajili vijana wakazi wa Hola

Kinara wa chama cha UGM, Neto aitaka IEBC isajili vijana wakazi wa Hola

Na KENYA NEWS AGENCY

KIONGOZI wa Chama cha United Green Movement (UGM) Agostino Neto ameitaka Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ianzishe mchakato wa usajili wa wapigakura huku ikisalia miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu kuandaliwa mwaka ujao.

Akizungumza mjini Hola baada ya kukutana na wanasiasa wanaopanga kukitumia chama hicho katika mwaka wa 2022, katika Kaunti ya Tana River, Bw Neto ambaye alikuwa mbunge wa zamani wa Ndhiwa, alisema IEBC inafaa ianze usajili huo na isiwaache vijana nyuma.

“Ni mwaka wa uchaguzi na vijana wengi bado hawajasajiliwa kama wapigakura, wengine nao hawana vitambulisho. IEBC inafaa iweke mikakati ya kuhakikisha usajili wa vijana kama wapigakura unaanza mara moja,” akasema Bw Neto.

Pia mwanasiasa huyo alimtaka Waziri wa Usalama wa Ndani, Dkt Fred Matiang’i ahakikishe kuwa vitambulisho vinatolewa kwa vijana kutoka kaunti za Garissa na Tana River ambao walituma maombi baada ya kutimu miaka 18.

Aidha, aliitaka IEBC pia kuwasajili Wakenya wanaoishi ng’ambo kama wapigakura.

 

You can share this post!

Wanasiasa wasukuma vijana wachukue vitambulisho

Raila na Mudavadi wamenyania kura za Magharibi