• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 2:08 PM
Joho na Mucheru waonya wakazi dhidi ya Ruto

Joho na Mucheru waonya wakazi dhidi ya Ruto

Na Winnie Atieno

WAZIRI wa Habari, Teknolojia na Mawasiliano (ICT) Joe Mucheru na Gavana Hassan Joho walimsuta na kumshambulia Naibu wa Rais William Ruto wakisema anaendesha siasa potovu za kuwahadaa vijana kuunga mkono azma yake.

Wawili hao walisema Bw Ruto anawachochea vijana badala ya kutoa muafaka wa changamoto zinazowakabili. Walisema mpango wake wa uchumi kwa wananchi ni ya kuwahadaa Wakenya kumuunga mkono.

“Huu ni wakati wa vijana, jitokezeni ili mpiganie nafasi za siasa. Mkichagua viongozi wachujeni, siasa ni kujipanga ndiyo maana sisi tumejipanga na Rais Uhuru Kenyatta, yule mwingine msimsikize anawahadaa. Hatuwezi kukubali nchi ichezewe,” alisema waziri huyo.

Akiongea eneo la Mombasa kwenye mkutano wa vijana wawili hao walimsuta Bw Ruto kwa kumdhalilisha Rais.Bw Joho naye aliwataka vijana kujitokeza na kupigania uongozi.

Alliwataka vijana kuwa makini na viongozi wabinafsi. “Tumesalia na miezi 11 kabla ya uchaguzi mkuu, chujeni mnachoambiwa. Suala la uchumi ambalo anatangaza kila mahali haiwezifanikishwa humu nchini. Jihusishe na viongozi bora ambao wanawatakia mema sio wale wanaopenda kukosoa bila kutoa jawabu,” alisema. Alimshutumu Bw Ruto kwa ‘kulumbana’ na Rais.

“Kwanini unapigana na Rais ambaye anaenda kustaafu? Unachochea wakenya, tunataka amani katika nchi ambayo watu wanaishi na uwiano. Inauma sana kuona kiongozi akichochea hisia na kuleta chuki na uhasama,” alisema.

Vijana walionywa dhidi ya kupokea hongo ili kuuza kura zao.Aliyekuwa afisa mkuu wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Bw Ezra Chiloba aliwataka vijana kugombea viti vya kisiasa.

“Nchi hii iko mikononi mwa vijana, ni wjaibu wenu kujitokeza na kugombea viti vya kisiasa,” alisema Bw Chiloba.

You can share this post!

MSIMU WA KUNUNUA BARAKA

Anaamini talanta ya kuigiza itasaidia wengi miaka ijayo