• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 5:55 AM
ODM yafanya uchaguzi wa wasimamizi tawi la Thika

ODM yafanya uchaguzi wa wasimamizi tawi la Thika

Na LAWRENCE ONGARO

HUKUn siasa za kutafuta uungwaji mkono zikiendelea kuchacha, chama cha Orange Democratic Movement (ODM) kimefanya uchaguzi wa wanachama wake kutoka kaunti ndogo ya Thika.

Baadhi ya maafisa wakuu waliochaguliwa kuendesha shughuli za chama ni mwenyekiti Andrew Ng’ang’a Wanjukira. Naibu wake ni Richard Kioni. Katibu ni Michael Orao huku naibu wake akiwa ni Anne Nyokabi. Mwekahazina ni Alice Juma ambaye naibu wake ni Albert Mugeni Osoro.

Katibu mpya wa ODM tawi la Thika aliyechaguliwa Bw Michael Orao alipokuwa akihutubia wanachama wa chama hicho mjini Thika. Picha/ Lawrence Ongaro

Katibu mtendaji ni John Dames akisaidiwa na Virginia Wanjiru. Mwenyekiti wa wanawake ni Bi Dinah Owago. Mwakilishi wa kikundi maalum ni Ageyio Ali Huyo. Mwakilishi wa vijana ni Kennedy Odoyo.

Wanakamati wa chama hicho ni Mumbi Ng’aru, Elizabeth Wanjiru Matere, David Mureka, Charles Gikaria, Mwaura Mbugua, Kagiri Gicia, Francis Ngunjiri, James Maina, Eunice Maluki.

Kiongozi wa vijana ni Kennedy Odoyo na naibu wake ni Simon Kinyanjui. Mwekahazina ni Japheth Onditi. Maslahi ya walemavu yanalindwa na Fresher Akinyi.

Katibu wa wanawake ni Silpa Anyango naye mwekahazina ni Rose Muhonja.

Mwenyekiti wa chama katika tawi hilo Bw Wanjukira aliwahimiza wanachama wote wa chama cha ODM wawe mstari wa mbele kukipigia debe kote katika Kaunti ya Kiambu.

“Sisi kama wanachama ni lazima tumpigie debe kinara mkuu wa ODM Bw Raila Odinga. Wakati huu kila mmoja ana jukumu la kuwarai watu wa Mlima Kenya kumpigia kura Bw Odinga,” alifafanua Bw Wanjukira.

Alisema wakati kampeni zitang’oa nanga, kila mmoja miongni mwao atakuwa na jukumu la “kumtetea ‘Baba’ bila kurudi nyuma.”

Alisema kutakuwa na propaganda nyingi kuhusu ubaya wa Raila lakini hayo yasiwatishe hata kidogo kwani kiongozi huyo tayari amewafanyia Wakenya mambo mengi.

Katibu wake Bw Orao aliwashauri wanachama wa ODM walio eneo hilo la Mlima Kenya wawe na msimamo mmoja bila kuyumbayumba.

” Iwapo umeamua kutetea chama cha ODM tafadhali fanya hivyo na moyo mmoja bila kuwa na wasiwasi,” alisema katibu huyo.

Alisema hivi karibuni kinara wa ODM atazuru maeneo mengi ya Mlima Kenya na kwa hivyo akifika “ni sharti wanachama wake waonyeshe umaarufu wao katika eneo hili la Mlima Kenya.”

You can share this post!

Pwani: Kiangazi chaleta maafa

ULIMBWENDE: Jinsi ya kutunza vidole na kucha