• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:55 AM
Mwaniaji kiti cha ubunge na mkewe watozwa faini kwa kughushi stakabadhi

Mwaniaji kiti cha ubunge na mkewe watozwa faini kwa kughushi stakabadhi

Na RICHARD MUNGUTI

MWANIAJI kiti cha ubunge Kimilili ametozwa faini ya Sh110,000 pamoja na mkewe kwa kughushi stakabadhi za umiliki wa kampuni.

Endapo Patrick Juma Kingoro na mkewe  Wilykster Ndanu Mwendwa hawatalipa faini hiyo watasukumwa jela miezi 22 kila mmoja.Walikiri mashtaka dhidi yao 11 ya kughushi stakabadhi za usajili wa kampuni ya Group Seven Security.

Wakijitetea washtakiwa hao walieleza mahakama wako tayari kurejesha kampuni hiyo kwa wenyewe.Ijapokuwa hakimu mkuu mahakama ya Milimani, Bi Martha Mutuku aliombwa awasukumie kifungo kikali washtakiwa hao walijitetea wakisema “wamiliki wa kampuni hiyo hawakupoteza chochote na tena wako tayari kuirejesha.”

Kiongozi wa mashtaka Bw Anderson Gikunda  alisema washtakiwa walighushi stakabadhi za kampuni hiyo 2017.Mahakama ilisema washtakiwa hao wameiondolea mahakama muda  wa kusikiza kesi hiyo.

Pia alisema mashahidi ambao wangeliitwa na upande wa mashtaka sasa hawatafika mahakamani.Walipewa siku 14 za kukata rufaa endapo hawakuridhika na adhabu.

  • Tags

You can share this post!

Ruto ataka wabunge wasipoteze muda wakifufua BBI

Tamaa yapelekea hoteli ya kifahari kufungwa