• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
Majangili wavamia kituo na kuiba bunduki

Majangili wavamia kituo na kuiba bunduki

Na JAMES MURIMI

MAJANGILI waliokuwa na silaha kali, Jumatatu walivamia kituo cha polisi katika Kaunti-ndogo ya Laikipia Kaskazini ambapo waliiba bunduki moja na sare za polisi.

Majangili wanne, wote waliokuwa na bunduki aina ya AK47, walivamia kituo hicho saa sita mchana na kuiba bunduki aina ya G3 na risasi kadhaa.

Mkuu wa polisi eneo la Laikipia North (OCPD), Ancent Kaloki Jumanne alisema majangili hao walimkabili konstebo Elisho Okoth Wasonga aliyekuwa katika ofisi ya kupokea ripoti katika kituo hicho.

“Majangili hao walimuamuru afisa huyo kuwapa bunduki ya G3 aliyokuwa nayo au wampige risasi. Afisa huyo aliwapa silaha hiyo na risasi 40 za milimita 7.62,” alisema Bw Kaloki kwa simu.

Kituo hicho kiko mkabala na kituo cha kibiashara cha Ewaso kilichoko kwenye mpaka wa Kaunti ndogo ya Isiolo North.

Mkuu huyo wa polisi pia alisema kwamba majangili hao walivunja nyumba ya Bw Okoth iliyo ndani ya kituo hicho na kuiba sare zake za polisi.

You can share this post!

West Ham wadengua Man-United kwenye raundi ya tatu ya...

Mawakili wa kesi ya Lenolkulal taabani