• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Watoto wa demu wadharau sponsa

Watoto wa demu wadharau sponsa

Na JOHN SAMUEL MUTUKU

BAHATI, NAKURU

POLO wa eneo hili aliyekuwa akijiandaa kuoa alipata mshangao atakaochukua muda mrefu kusahau maishani mwake baada ya kumtembelea mchumba wake na badala ya kukaribishwa, akadharauliwa na watoto.

Jamaa aligundua demu aliyekuwa akimhadaa hana watoto na hajawahi kuolewa, alikuwa mama wa watoto wanne na alikuwa ametorokwa na mumewe ambaye alikuwa tajiri.

Vile vile, mwanadada alikuwa akibadilisha wanaume na hata kuwapeleka nyumbani na kuwatambulisha kwa watoto wake kama baba yao.

Kulingana na mdokezi jamaa alikutana na demu mjini Nakuru na baada ya kuchumbiana kwa miezi kadhaa, wakaamua kwenda kwa demu.

Polo alijiona wa maana sana akiendesha gari. Walipofika nyumbani kwa demu, polo alikaribishwa na watoto wanne waliovalia mavazi mazuri mazuri.

“Hawa ni kina nani?” polo alimuuliza demu wakiwa bado ndani ya gari.

“Hawa watoto smart ni wa dadangu ambaye hufanya kazi jijini Nairobi. Usione ajabu wakiniita mum,” demu alieleza akitabasamu.

Mum, huyu ni dad wa aina gani umetuletea?” mmoja aliuliza polo alipotoka katika gari.

“Tazama anaendesha probox, gari lisilo zuri kama la dad wa kwanza,” mtoto wa pili alisema.

“Na hata mavazi yake si mazuri kama yule dad aliyetutoroka,” wa tatu naye alishindwa kunyamaza.

“Kwa hivyo wewe ndiwe mama wa watoto hawa ilhali umekuwa ukinidanganya hujawahi kupata mtoto hata mmoja?” polo alishangaa.

Badala ya kuingia ndani ya nyumba, polo aliingia katika probox yake na kuondoka mbio mbio.

“Itakuwa vigumu kuwaamini kina dada wa siku hizi. Baadhi yao ni mashetani wakubwa,” jamaa alisikika akiambia rafiki yake.

 

You can share this post!

TAHARIRI: TSC idhibiti zogo la shule haraka

Kikosi cha Uganda chawasili kwa mechi ya kufuzu kushiriki...