• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
Jifunze kuoka keki ya kakao na vanilla

Jifunze kuoka keki ya kakao na vanilla

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Muda wa mapishi: Dakika 50

Walaji: 5

Vinavyohitajika

  • siagi robo kilo
  • sukari robo kilo
  • unga robo kilo
  • mayai 6
  • arki ya vanilla kijiko 1
  • kakao yaani cocoa vijiko 3
  • baking powder 1
  • chungwa 1
  • maganda ya chungwa kijiko 1
  • chumvi

Maelekezo

Chekecha unga kwenye bakuli kisha weka chumvi na baking powder na uchanganye vizuri kwa mwiko.

Osha chungwa vizuri kisha lipare kwa kipario ili upate maganda yake kijiko kimoja. Weka maganda ya chungwa kwenye unga na uchanganye tena vizuri.

Weka sukari na siagi kwenye bakuli jingine.

Saga mchanganyiko wako kwa muda wa dakika tatu (3).

Weka Vanilla endelea kusaga kwa muda wa dakika mbili (2).

Weka mayai yako moja baada ya jingine mpaka uyamalize huku ukiendelea kusaga.

Weka juisi ya chungwa kisha saga tena kidogo.

Malizia kuweka unga kidogo kidogo mpaka umalize wote huku ukisaga.

Chukua bakuli gawa mchanganyiko wako kisha weka kakao (cocoa) kwenye bakuli ul’oweka mchanganyiko wako halafu changanya vizuri kwa kijiko kikubwa.

Washa ovena nyuzi joto sentigredi 160. Chukua chombo chako cha kuokea, kisha anza kuweka mchanganyiko mweupe na kati weka wa cocoa kisha malizia mweupe.

Oka kwa dakika 50 kisha fungua jiko na tazama keki yako.

Ingiza kijiti au kisu safi kwenye sehemu mbali mbali – tofauti – za keki yako kuangalia kama imeiva.

Ikiwa kijiti kitatoka na umaji maji basi keki yako bado rudisha kwenye ovena.

Ikipoa toa kwenye trei na ikate vipande tayari kuliwa na kinywaji upendacho.

You can share this post!

TAHARIRI: Sakata ya Kemsa inakatisha tamaa

Olunga afunga mabao 5 kuisaidia Al Duhail kuzamisha Al...