• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Ujanja wa kahaba wazimwa na mganga

Ujanja wa kahaba wazimwa na mganga

Na JOHN MUTUKU SAMUEL

DEMU aliyesifika mtaani hapa kwa ujanja wake wa kuwatapeli wanaume maelfu ya pesa baada ya kula uroda nao, alibanwa asijue la kufanya baada ya kukutana ana kwa ana na mjanja wa wajanja.

“Kisu kimegusana na mfupa! Hapa kwangu utakula huu na hasara juu. Ondoka sasa ama niambie ‘vijana’ wangu wakufanyie kazi,” demu alitishwa na jamaa aliyelenga kumpora.

Demu ambaye alikuwa akifanya kazi ya ukahaba alikuwa ametafuna pesa za wanaume kwelikweli.

Kila alipotembea na mwanamume, alimtisha kwa kisu na kudai kulipwa pesa nyingi. Mwanamume aliyekosa pesa alinyang’anywa simu au chochote cha thamani ndani ya nyumba.

Siku ya arubaini ya demu ilipofika, alikutana na polo katika baa usiku.

Walikata maji kisha polo akaamua kumpeleka kwake. Walikula uroda usiku kucha kisha alfajiri, demu akadai alipwe Sh5,000. Polo alikuwa na Sh500 pekee mfukoni.

“Nitoe wapi pesa hizo jamani? Nina Sh500 tu!” Polo alimpasulia mbarika.

“Utajua hujui! Unajua unacheza na nani wewe? Mimi huminya mwanamume akanipigia magoti na kunililia,” demu alimtisha akimrushia kofi lakini likadakwa.

“Leo umepatana na dume lisiloogopa visu wala bastola. Tazama humu kabatini. Waona nini?” polo alimfungulia kabati.

Demu alishangaa kuona mifupa mingi ya aina tofauti, jambo lililomtia woga usio wa kawaida.

“Ukiendelea kunitishatisha, hutatoka katika nyumba hii. Nitahakikisha umekuwa chizi,” polo ambaye alikuwa mganga alimlipukia demu.

Demu aliondoka polepole akafungua mlango na kutoweka bila kutazama nyuma tena.

Aliapa kutokanyaga kwa polo tena akijua fika kuwa pwagu hupata pwaguzi.

You can share this post!

Arsenal na Palace watoshana nguvu katika gozi la EPL ugani...

PATA USHAURI WA DKT FLO: Nitashikaje mimba ya mtoto mvulana?

T L