Faida za kiafya za oregano

Faida za kiafya za oregano

NA MARGARET MAINA

mwmaina@ke.nationmedia.com

OREGANO au majorama mtamu huchukuliwa kuwa miongoni mwa mimea muhimu katika vyakula vingi duniani kote.

Kwa kawaida oregano hupatikana ama ikiwa mbichi, iliyokaushwa au kama mafuta, na aina hizi zote huwa na manufaa makubwa kiafya.

Ingawa hutumiwa kwa kiasi kidogo, oregano hupakia baadhi ya virutubisho muhimu.

Oregano ina kemikali ambazo zinaweza kusaidia kupunguza kikohozi. Oregano pia inaweza kusaidia katika usagaji chakula na kupambana na baadhi ya bakteria na virusi. Watu hutumia oregano kwa uponyaji wa jeraha, maambukizi ya vimelea, na hali nyingine nyingi.

Kukabili radikali hatari mwilini

Oregano huwa na misombo ya kusaidia katika kupambana na uharibifu kutoka kwa radikali hatari mwilini.

Kwa pamoja na matunda na mboga, oregano husaidia kuboresha afya yako.

Inaweza kusaidia kupunguza maambukizi ya virusi

Mbali na kupigana na bakteria, oregano na vijenzi vyake vinaweza pia kulinda dhidi ya virusi kadhaa kama maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuhara, kichefuchefu na maumivu ya tumbo.

Inaweza kupunguza kuvimba

Uvimbe unaotokea baada ya ugonjwa au kuumia unaweza kudhibitiwa lakini ukigeuka uvimbe sugu unaweza kuchangia ukuaji wa magonjwa kama vile ugonjwa wa moyo, kisukari na kudorora kwa kinga ya mwili.

Oregano ina misombo muhimu inayoweza kusaidia kupunguza radikali hatari na kupunguza kuvimba.

Ni rahisi kuongeza kwenye mlo wako

Ingawa unaweza kufikiria oregano kama kiongezo tu kwa pizza na sahani za pasta, mimea hii inaweza kutumika kwa njia nyingi.

Jaribu kuchanganya majani yote ya oregano kwenye mboga nyingine ili kuandaa saladi iliyojaa virutubisho au kunyunyiza majani ya oregano kwenye pilipili, supu au kitoweo. Unaweza pia kuitumia kwenye kitoweo cha nyama.

Oregano inapatikana mbichi, kavu au kama mafuta, na kuifanya iwe rahisi sana kuiongeza kwenye lishe yako.

Inaboresha afya ya utumbo

Hali ya kimwili na kazi ya fiziolojia ya sehemu mbalimbali za njia ya utumbo ni afya ya utumbo. Mazingira machafu, kama vile chakula na maji yaliyochafuliwa, hutoa fursa ya uvamizi wa vimelea kwenye utumbo na kusababisha magonjwa mbalimbali.

Kutumia mafuta ya oregano kunaweza kusababisha vimelea kutoweka kabisa.

  • Tags

You can share this post!

Jicho Pevu aponea shambulio la risasi

AFYA: Vidokezo vya jinsi ya kupunguza ‘uzito wa...

T L