• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Ashtakiwa kwa madai ya kusaidia mtoto kuavya mimba

Ashtakiwa kwa madai ya kusaidia mtoto kuavya mimba

NA BRIAN OCHARO

MWANAFAMASIA ameshtakiwa kwa madai ya kuuzia dawa msichana mwenye umri wa miaka 15 ili kuavya mimba.

Bw Amos Nzioki Mutinda, Jumanne, Juni 6, 2023 alifikishwa mbele ya mahakama ya Mombasa kuhusu kosa hilo alilodaiwa kutenda katika eneo la Tudor.

Hati ya mashtaka inadai kuwa, mshukiwa alisambaza dawa hizo kinyume cha sheria kwa mtoto huyo kwa nia ya kumsaidia kuavya mimba.

Bw Mutinda hata hivyo alikanusha kosa hilo alipofika mbele ya Hakimu Mkuu Martha Mutuku.

Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh300, 000 na mdhamini mmoja wa kiasi sawa na hicho.

Mahakama iliambiwa kuwa, mwathiriwa alimwendea mshukiwa ili kumsaidia kuavya mimba.

Rekodi ya mahakama ilionyesha kuwa shuguli hiyo ilifanyika mwendo wa saa tatu usiku.

Rekodi za polisi pia zilionyesha kuwa msichana huyo alikuwa amenajisiwa kati ya Januari na Machi mwaka huu, 2023.

Kesi hiyo itatajwa Juni 14.

 

  • Tags

You can share this post!

KASHESHE: Betty Kyalo azungumzia ndoa yake iliyovunjika

Jackson Mutiso ashinda Sh20 milioni za SportPesa Midweek...

T L