• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 10:55 AM
DPP ataka kesi za Kimwarer, Arror ziunganishwe

DPP ataka kesi za Kimwarer, Arror ziunganishwe

Na RICHARD MUNGUTI

MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP), Noordin Haji sasa anataka kesi za ufisadi wa Sh63 bilioni zinazowakabili aliyekuwa waziri wa Fedha Henry Rotich na mkurugenzi mkuu wa zamani Shirika la Ustawi wa Kerio Valley (KVDA), David Kimosop ziunganishwe.

Kesi hizo mbili zinahusu kufujwa kwa pesa katika ujenzi wa mabwawa ya Kimwarer na Arror.

Katika ombi hilo, DPP amepunguza idadi ya washtakiwa kutoka 18 hadi tisa.

Pia amepunguza mashtaka kutoka 40 hadi 30.

Akiwasilisha ombi hilo, kiongozi maalum wa mashtaka, Bw Taib Ali Taib na naibu wa DPP, Bw Alexander Muteti, walimweleza Hakimu Mkuu wa mahakama ya Milimani, Bw Lawrence Mugambi, kuwa idadi ya mashahidi imepunguzwa kutoka 104 hadi 52.

“Lengo la kuwasilisha ombi hili la kuunganishwa kwa kesi hizi mbili dhidi ya Bw Rotich na Bw Kimosop ni kuhakikisha imekamilishwa kwa haraka,” alisema Bw Muteti.

Kesi hiyo itatajwa tena Oktoba 26.

You can share this post!

Miraa: Raila aahidi kutafutia wakuzaji soko akiingia ikulu

Kanu yaimarisha kampeni mashinani

T L