NA MAUREEN ONGALA
MBUNGE wa Ganze Kenneth Kazungu amelitaka Shirika la Huduma kwa Wanyamapori (KWS) kurudisha huduma zake mashinani ili kupunguza mahangaiko ya wananchi ambao makazi yao na mashamba yamevamiwa na ndovu.
Amelalamika imekuwa vigumu kwa waathiriwa wa uvamizi wa wanyamapori kupata fidia kwa sababu ya gharama za kusafiri hadi afisi za KWS mjini Malindi.
Chifu wa Mrima wa Ndege, Bw Samson Chai, alisema wakulima pia wanalazimika kugharimia usafiri wa afisa wa kilimo kuja kukagua hasara wakati ndovu wanavamia mashamba yao.
Wadi zilizoathirika zaidi ni Bamba, Ganze na Sokoke.