Na RICHARD MUNGUTI
MMISHENARI kutoka Canada ameshtakiwa kwa ulaghai wa shamba la Sh60 milioni.
Sheppard Nelson Jason aliyeshtakiwa mbele ya mahakama ya Milimani alikana mashtaka matano ya kula njama za kumnyang’anya Jeremiah Muuya Sailoji na mkewe Rhodah Anne Baxter shamba la ektari 6.5.
Alikana mashtaka mbele ya hakimu mkuu Lucas Onyina.
Jason aliomba hakimu amwachilie kwa dhamana akisema “amekuwa akiishi hapa nchini kwa zaidi ya miaka10 na hawezi kutoroka.”
Mshtakiwa alieleza mahakama amejenga makao ya watoto na anawasaidia watoto mayatima 85 wanaoishu katika shamba hilo.
Upande wa mashtaka haukupinga mshtakiwa akiachiliwa kwa dhamana.
Hakimu Onyina alimwachilia kwa dhamana ya Sh200, 000.