Na RICHARD MUNGUTI
MTUNZAJI jengo la makazi mtaani Umoja Nairobi ameshtakiwa kwa kumnajisi mwanamke mwenye akili punguani, huku akimuahidi atamnunulia “Chapatti”
Daniel Waka mwenye umri wa miaka 51 adaiwa alimtendea dhuluma za kimapenzi mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 38 katika paa la jengo analolitunza.
Waka anakabiliwa na shtaka badala la kumpapasa papasa mlalamishi sehemu nyeti kinyume na sheria nambari 11 za SOA.
Upande wa mashtaka unasema mshtakiwa alimvamia mlalamishi akianika nguo.
Mlalamishi anayeishi na watu wa familia yake alikuwa ameonywa na mshtakiwa asitoboe siri yao, huku akimuahidi atakuwa anamnunulia “chapatti kila wakati.”
Kiongozi wa mashtaka alimweleza hakimu kwamba mlalamishi hawezi kumbuka siku na tarehe aliyodhulumiwa kimapenzi lakini ni Machi 2023.
Mshtakiwa aliachiliwa kwa dhamana ya Sh100,000.
Kesi hiyo itasikizwa Septemba 27, 2023.
Upande wa mashtaka uliagizwa umkabidhi mshtakiwa nakala za mashahidi aandae tetesi zake.