NA WACHIRA MWANGI
WAPANGAJI wa nyumba za Buxton jijini Mombasa wanamtaka Rais William Ruto aingilie kati suala lao la kuhamia kwa nyumba za kisasa eneo la Buxton Point.
Kulingana na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wapangaji hao Bw John Tsuma, wapangaji hao wanataka Rais Ruto aingilie kati mpango wa kuwapa makazi mapya katika mradi mpya wa ujenzi jinsi walivyoahidiwa.
Wakizungumza nje ya Hospitali ya Rufaa ya Coast General walipoenda kumuaga mwendazake Patrick Mucheru, wapangaji hao walisema ni wamadhulumiwa kwa sababu kila mmoja ameambiwa alipe Sh4 millioni ili aweze kumiliki nyumba.
Waliibua madai kuwa wenzao wanaaga dunia kwa sababu ya msongo wa mawazo.