NA SAMMY WAWERU
RAIS William Ruto Alhamisi, Juni 1, 2023 ataongoza taifa kuadhimisha Sikukuu ya Madaraka Dei 2023.
Ni siku maalum inayoadhimishwa Juni 1 kila mwaka kusherehekea uhuru wa ndani kwa ndani Kenya kujitawala, kutoka kwa serikali ya Mbeberu.
Maadhimisho ya 2023 yananyika katika Uwanja wa Moi, Embu.
Wananchi kutoka sehemu mbalimbali za nchi, walianza kufurika uwanjani humo alfajiri na mapema, usalama ukiimarishwa ndani na nje.
Maadhimisho sawa na hayo, yanatarajiwa kufanyika katika kiwango cha kaunti chini ya uongozi wa magavana.