• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Madaraka Dei Juni 1, 2023

Madaraka Dei Juni 1, 2023

NA SAMMY WAWERU

RAIS William Ruto Alhamisi, Juni 1, 2023 ataongoza taifa kuadhimisha Sikukuu ya Madaraka Dei 2023.

Wananchi wakiingia Uwanja wa Moi, Embu. Picha / CHARLES WANYORO

Ni siku maalum inayoadhimishwa Juni 1 kila mwaka kusherehekea uhuru wa ndani kwa ndani Kenya kujitawala, kutoka kwa serikali ya Mbeberu.

Mwananchi akikaguliwa kuingia Uwanja wa Moi, Embu. Picha / CHARLES WANYORO

Maadhimisho ya 2023 yananyika katika Uwanja wa Moi, Embu.

Askari akikagua mkoba wa mama ili aruhusiwe kuingia Uwanja wa Moi, Embu. Picha / CHARLES WANYORO

Wananchi kutoka sehemu mbalimbali za nchi, walianza kufurika uwanjani humo alfajiri na mapema, usalama ukiimarishwa ndani na nje.

Afisa wa kijeshi, KDF, akilinda kiingilio cha watu mashuhuri Uwanja wa Moi, Embu. Picha / CHARLES WANYORO

Maadhimisho sawa na hayo, yanatarajiwa kufanyika katika kiwango cha kaunti chini ya uongozi wa magavana.

Kiingilio cha watu mashuhuri Uwanja wa Moi, Embu. Picha / CHARLES WANYORO
  • Tags

You can share this post!

Mzee wa jamii ya Boni adai hakuna cha kujivunia Madaraka Dei

Maadhimisho ya Madaraka Dei Juni 1, 2023, katika Uwanja wa...

T L