• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Mtoto niliyempata anakuja na bahati ya ushindi – Mgombea

Mtoto niliyempata anakuja na bahati ya ushindi – Mgombea

NA AFP

BANGKOK, Thailand

MMOJA wa wale wanaopigiwa upatu kushinda katika uchaguzi mkuu wa Thailand jana Jumatano alitaja mwanawe mchanga kama “silaha ya kisiri” alipowasilisha mtoto huyo wa kiume kwa wanahabari baada ya kujifungua wiki mbili kabla ya siku ya kura.

Paetongtarn Shinawatra, binti ya Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand, Thaksin Shinawatra, aliapa kurejea kampeni kuelekea uchaguzi utakaofanyika Mei 14. Alijifungua mtoto huyo wa kiume mnamo Jumatatu.

Shinawatra, 36, ameshikilia nambari moja au mbili katika kura za utafiti wa maoni kuhusu nani anapendelewa na wapigakura wengi kuwa Waziri Mkuu.

Aidha, chama chake, Pheu Thai Party, chenye sifa za vuguvugu lililoanzishwa na babake, kinaongoza katika kura za maoni zilizoendeshwa na mashirika mengi ya utafiti.

“Naamini vitu vizuri huja na watoto, kwa hivyo hii ni baraka kwa familia yangu,” Shinawatra aliwaambia wanahabari katika hospitali ya Praram 9 jijini Bangkok.

“Watoto wangu ni siri yangu ya nguvu ya kufanya na kuishi maisha,” akaongeza.

Tafsiri: CHARLES WASONGA

  • Tags

You can share this post!

Eritrea yafungua mipaka yake kuruhusu wakimbizi wa...

TAHARIRI: Wahalifu wote wa mauaji ya Shakahola wafichuliwe...

T L