• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 7:50 AM
Akothee na Jaguar wakabana koo kuhusu utajiri

Akothee na Jaguar wakabana koo kuhusu utajiri

NA MERCY KOSKEI

WAZIRI msaidizi (CAS) Charles Njagua almaarufu Jaguar na mwimbaji Esther Akoth – Akothee wameendelea kupimana nguvu nani ndiye tajiri zaidi kuliko mwenzake.

Alipokua akijibu matamishi ya Akothee kuhusu nani yuko juu ya mwingine kifedha, Jaguar alisuta utajiri wa Akothee akidai kuwa hakustahili kuwa juu yake kwenye orodha hiyo.

Mwimbaji huyo alisema kwamba ikiwa Akothee na Harmonize ni tajiri zaidi yake, atastaafu kwenye muziki na pia kujiuzulu kutoka kwa wadhifa wake serikalini.

“Ukiangalia orodha hiyo nimekuwa kwenye muziki  kwa zaidi ya miaka 15. Lakini naapa ikiwa Akothee na Harmonize ni matajiri kuliko mimi, nitawacha muziki. Wanachagua vitu wanavyoviona kama magari ya kifahari aina ya Range Rovers. Nimefanya mambo mengi, sijisifu,” Jaguar alisema.

Akimjibu, Akothee alimkashifu mwanasiasa huyo kwa majivuno yake, akimtaka awe mnyenyekevu na ajiepushe kwa kile alichosema ni “kujisifu na pesa za walipa kodi.’

“Mwanasiasa yeyote anayejisifu na pesa za walipa kodi na utajiri… Utajiri kitu Gani? Hizo tiketi za ndege na helikopta zinalipwa na serikali sio pesa zako binafsi!” aliandika kwenye mtandao wake wa Instagram.

“Mnajigamba ilhali watoto wa wananchi waliowaweka serikalini hawawezi kumudu karo ya shule. Msaada huu wote mnaofanya mtandaoni ni wa kujitengenezea jina. Kila mara mnasubiri kitu kinachovuma ili kugonga vichwa vya habari kwa sababu siku zote huna umuhimu wowote!”

Akothee, kwa majibu yake aliendelea kushangazwa na Jaguar na kumkashifu kwa kuanzisha vita “na mwanamke”.

“Mwanaume yeyote akijilinganisha na wanawake ana tatizo la utambulisho. Nitawatandika mnikome,” alichapisha.

Jaguar, kupitia Instagram amemtaka Akothee kuepuka na kumshambulia akisema kuwa la sivyo atakabiliana na yeye akisema kuwa atapenda hatima yake.

Akitumia maneno ya mhubiri tata Paul Mackenzie, Jaguar  alimwambia “Unachokipigania hukijui, kitakuramba Akothee,” alichapisha kwenye mtandao wake wa Instagram.

Haya yanajiri wakati Konde Boy Harmonize amemkashifu Jaguar kwa maneno yake ambayo, bila shaka, hayakukaa naye vyema.

Katika majibu yake, Harmonize alisema kuwa angekuwa Jaguar, angekuwa tayari ameshastaafu muziki.

 

  • Tags

You can share this post!

Alai na Sonko wavuana mashati mtandaoni

Miguna Miguna aponda wanahabari

T L