• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Akothee: Sijashika mimba ya ‘Omosh’ kwa sababu ya msongo wa mawazo

Akothee: Sijashika mimba ya ‘Omosh’ kwa sababu ya msongo wa mawazo

Na MWANDISHI WETU

MWANAMUZIKI Esther Akoth maarufu kama Akothee amefunguka kwa nini bado hajashika mimba ya bwanake Dennis Schweizer (Omosh).

Akothee ambaye tayari ana watoto watano, alisema kuwa huenda anatatizwa na msongo wa mawazo ndio maana amechelewa kushika mimba.

Akiandika kuhusu ndoa yake kwenye ukurasa wake wa kijamii wa Instagram, mwanabiashara huyo alieleza kuwa hakuweza kufurahia fungate kwani bwanake alirudi kazini baada ya kufunga ndoa.

“Itabidi nishughulike na mapenzi yangu kwani daktari wangu aliniarifu kuwa kupanga harusi huwa kunachosha na ninaweza kosa kushika mimba hivi karibuni,” akaeleza.

Vile vile, aliwaomba mashabiki wake kumpa muda wa kumtafuta mtoto wake wa sita kwani ananuia kuwa mama mwaka huu.

“Nitachukua muda kutoka mitandao wa kijamii na watu ili niweze kumtafuta mtoto wangu wa sita kabla tuzungumzie mambo mengine. Bwana yangu alisema niondoke mitandaoni, niwache kufanya kazi na nisafiri nje ya nchi kabla Ijumaa,” akaongezea.

Akothee ananuia kufanya harusi nyingine ifikapo Julai nyumbani kwa mpenziwe Uswizi.

Mwanamuziki huyo alifunga ndoa wakati wa siku yake ya kuzaliwa Aprili 10, 2023 karika sherehe kubwa iliyowajumuisha wanasiasa na watu tajika na mashuhuri nchini.

Harusi yake iliyokuwa ya kukata na shoka ilienea mitandaoni kwa siku kadhaa, huku wengi wakimsifia kwa kuolewa tena.

Alisema kuwa aliwahi kuolewa tena na hata ingawa ndoa hizo hazikufanikiwa, anashukuru baba watoto wake kwa kumpa watoto anaowaenzi.

Alipokuwa akisherehekea mwezi mmoja tangu kuolewa, Akothee aliwaomba mashabiki wake kumpigia makofi kwa kuvumilia ndoa kwa mwezi huo mmoja.

Akothee anajulikana kwa kuchamba na kuzungumza yaliyo moyoni pasi uoga au wasiwasi.

Hii imemfanya kupata marafiki na maadui wengi lakini hababaishwi.

Hivi majuzi, Akothee alimpasha Waziri msaidizi (CAS) Charles Kanyi almaarufu Jaguar kwa kusema kuwa yeye ndiye mwanamuziki mwenye pesa nyingi nchini.

Hata ingawa wawili hawa walitupiana maneno mtandaoni, Akothee alimsuta Jaguar akisema kuwa ametajirishwa na kazi ya serikali na anapaswa kumshukuru Rais William Ruto kwa kumteua kama Waziri msaidizi.

  • Tags

You can share this post!

BORESHA AFYA: Viungo vizuri kwa afya yako

Zingatia mambo haya uishi na watu vizuri

T L