• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 1:08 PM
KASHESHE: Betty Kyalo azungumzia ndoa yake iliyovunjika

KASHESHE: Betty Kyalo azungumzia ndoa yake iliyovunjika

NA JOHN KIMWERE

MWANABAHARI Betty Kyalo ameshikilia kuwa bado hawezi kueleza kilichochangia kuvunjika kwa ndoa yake na aliyekuwa mumewe Dennis Okari.

Ndoa yake na mwanabahari mwezake ilivunjika mwaka 2016, ikiwa ni miezi sita tu baada ya kufunga pingu za maisha katika hafla ya kufana iliyoandaliwa mtaani Karen jijini Nairobi.

Wawili hao walikuwa wamechumbiani kwa muda wa miaka minne. Betty akizungumza kwenye kipindi cha Wicked Edition katika kinachopeperushwa na kituo cha runinga cha NTV alisema kamwe hafahamu kilichotendaka.

”Mimi huwaza na kuwazua kutafuta sababu iliyofanya ndoa yangu kuvunjika lakini wapi! Hushindwa kuelewa,” alisema.

Ingawa hivyo, anashikilia kuwa kama haiwezekani, haiwezekani… Hakuna cha kulazimisha. Betty, 34 na mzazi mwenzake, Okari kwa sasa kila mmoja anaendelea na maisha yake huku ikifahamika mwenzake ameshapata jiko.

Kutengana kwa wawili hao kuliwaacha Wakenya wengi midomo wazi kwa kuzingatia harusi yao iliyogharimu fedha nyingi sana.

Mwaka 2022, Betty aliweka wazi kuwa licha ya ndoa yao kugonga ukuta, hawana uhasama wowote na huwa wanashirikiana vizuri katika malezi ya binti yao mwenye umri wa miaka minne.

Alisema kuwa yeye na mzazi mwenzake huwa wanazungumza kupitia simu vizuri tu hata huwa wanahudhuria mikutano ya shule ya mwana wao, hali ambayo huchangia watu wengi kudhania kwamba bado wapo pamoja.

Alidokeza kuwa Okari anapenda sana binti yao na kila mmoja huwa anapata muda mwafaka kukaa naye. Pia alifunguka kuwa binti yao anapenda sana babake.

  • Tags

You can share this post!

Msitu wa Shakahola kuwa eneo la makumbusho ya tukio la...

Ashtakiwa kwa madai ya kusaidia mtoto kuavya mimba

T L