NA MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 10
Muda wa mapishi: Dakika 30
Walaji: 2
Vinavyohitajika
Maelekezo
Hatua ya kwanza ni kuhakikisha una githeri (mchanganyiko wa mahindi na maharagwe) kilichochemshwa tayari. Unaweza kutumia aina yoyote ya maharagwe.
Weka mafuta na chumvi kwenye sufuria yako. Acha hii ifuatwe na mashina ya dania, vipande vya kitunguu chekundu na pilipili mboga. Harufu itakua nzuri sana katika hatua hii.
Viive kwenye moto mdogo hadi viwe laini na vyenye harufu nzuri kabla ya kuongeza nyanya na viungo.
Ongeza maji kidogo (au mchuzi wa mboga), kisha chemsha kwenye moto mdogo kwa dakika chache. Usikimbilie kuepua kwa sababu viungo vinahitaji kuyeyushwa na mchuzi kuwa mzito.
Unaweza kuweka viazi kwenye githeri ikiwa unapenda. Ongeza viazi na upike kwa muda mchache tu ili viazi visiive kabisa.
Baada ya hayo, ongeza mahindi ya kuchemsha na maharagwe kisha karoti (pia kata vipande vidogo), na kuruhusu kila kitu kichemke kwenye moto mdogo hadi vyote viive. Hii itachukua dakika chache.
Pamba kwa majani ya giligilani iliyokatwakatwa kisha chukua parachichi uongezee ikiwa unapenda. Pakua na ufurahie chakula chako.