NA MARGARET MAINA
SHAKSHUKA ni mlo unaoweza kutengeneza kwenye sufuria ukitumia mayai yaliyowekwa katika mchuzi wa nyanya, viungo na pilipili.
Ni chakula kitamu kuliwa kama kiamsha kinywa au kama chakula cha jioni, na hushibisha wakati wowote wa siku. Mlo huu unahusu nyanya. Tumia nyanya zilizosagwa na ambazo ni za ubora zaidi unazoweza kupata.
Muda wa kuandaa: Dakika 10
Muda wa mapishi: Dakika 20
Walaji: 2
Vinavyohitajika
Maelekezo
Kwenye sufuria kubwa au pana, juu ya moto wa kati, pasha mafuta hadi yaanze kutoa moshi.
Ongeza kwa uangalifu nyanya za cherry na pilipili mboga kwenye mafuta ya moto.
Pika kwa dakika kadhaa huku ukikoroga mara moja au mbili hadi vianze kuwa kama vina malengelenge na rangi ya hudhurungi.
Ongeza kitunguu saumu na mbegu za jira na ukoroge kila mara kwa muda wa sekunde 15 au mpaka kitunguu saumu kiwe na harufu nzuri.
Ongeza vitunguu maji vilivyokatwa, na endelea kupika huku ukikoroga hadi vitunguu viive tuseme baada ya dakika tatu au nne.
Ongezea na changanya kwa upole viazi, nyanya iliyokatwa, paprika na chumvi. Punguza moto hadi wastani, na pika huku ukichochea hadi mchanganyiko uwe mzito kidogo. Itakuchukua kama dakika tano hivi.
Upe mchanganyiko wa nyanya ladha kabla ya kuendelea na hatua inayofuata, na uongeze chumvi zaidi ikiwa unataka.
Tumia kijiko kufanya mashimo sita ya kina katika mchanganyiko wa nyanya. Vunjia yai moja moja ndani ya kila shimo halafu funika sufuria, na upike kwa muda wa dakika tano au hadi mayai yaive. Ondoa kutoka kwa moto.
Nyunyizia majani ya giligilani na jibini juu, pakua na ufurahie.