NA MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 10
Muda w amapishi: Dakika 15
Walaji: 2
Vinavyohitajika
Vidokezo kuhusu viungo:
Kiasi cha viungo hivi vyote kinaweza kutofautiana kwa kutegemea ladha yako au jinsi unavyopenda.
Unaweza kutumia mafuta mengine yoyote ya kukaangia: mafuta ya alizeti, mafuta ya mboga na kadhalika.
Maelekezo
Chambua viazi na ukate viwe kwa umbo la diski nene. Kata vitunguu. Kata pilipili mboga kisha suuza majani ya mchicha.
Chemsha maji kidogo, ongeza viazi vilivyokatwa na upike kwenye moto wa juu kwa dakika tano.
Piga na uyakoroge mayai kwenye bakuli.
Ongeza pilipili, mbaazi za kijani, vitunguu na chumvi. Koroga vizuri sana.
Mimina mafuta ya mzeituni kwenye kikaangio na yanapopata moto, mimina mchanganyiko wa yai na ueneze.
Laza majani ya mchicha na vipande vya viazi kwenye yai, hakikisha kwamba viazi na mchicha vinatumbukizwa kwenye yai.
Funika, punguza moto uwe kwa kiwango cha chini sana na kaanga polepole kwa dakika 15 hadi 20 au mpaka yai lote liive bila kuungua.
Epua, pakua na ufurahie, unaweza kula kimanda kikiwa pekee au na maji ya matunda au na chochote ukipendacho.
Mambo muhimu ya kuzingatia
Tia chumvi kwenye mayai kabla ya kuyapika – Hii husaidia kuhifadhi unyevu wakati wa kupika.
Ongeza poda ya kuoka kwenye mchanganyiko wa yai – Kiasi kidogo cha poda ya kuoka (takriban ¼ kijiko) kwenye mayai. Hii ni hiari.
Epuka kuyapika kwa muda mrefu sana hadi yageuke kuwa kahawia sana kwani mayai yatakuwa yameiva kupita kiasi.