• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 2:08 PM
MAPISHI KIKWETU: Nyama ya kuku choma iliyoandaliwa kwa pamoja na kitunguu saumu na siagi

MAPISHI KIKWETU: Nyama ya kuku choma iliyoandaliwa kwa pamoja na kitunguu saumu na siagi

NA MARGARET MAINA

[email protected]

KUKU choma inapochomwa pamoja na siagi, kitunguu saumu, halwaridi, na limau huwa na ladha ya kipekee.

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa mapishi: Saa 1

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • kuku 1
  • limau kubwa iliyokatwa katikati
  • kikombe ½ cha siagi
  • chumvi
  • pilipili kwa ladha
  • vijiko 2 vya kitunguu saumu kilichomenywa
  • kijiko 1 vya zaatari, au ½ tsp kavu
  • vijiko 2 vya halwaridi
  • poda ya vitunguu
  • mafuta ya kupikia

Maelekezo

Washa ovena kwenye kiwango cha joto la nyuzijoto 200 kwa dakika 15.

Osha na ukaushe kuku kwa kitambaa cha karatasi.

Changanya mafuta ya mzeituni, siagi iliyoyeyuka, divai (ikiwa unatumia) na maji ya limau pamoja, kisha sugua mchanganyiko huu kwenye kuku kote, chini ya ngozi.

Weka nusu ya limau, vitunguu maji ndani ya kuku pamoja na matawi ya halwaridi. Unaweza pia kutumia zaatari au mimea mingine yoyote.

Funga miguu pamoja na kipande cha kamba ya jikoni na uweke mbawa chini ya kuku.

Nyunyuzia kwa juu chumvi na pilipili halafu paka kitunguu saumu juu ya kuku na chini ya ngozi.

Oka katika ovena iliyowashwa hadi nyuzijoto 200 kwa dakika 50. Ngozi ya kuku itakuwa ni ya kahawia ya dhahabu. Funika kuku kwa foil ya alumini na uendelee kuoka kwa dakika 30 zaidi.

Epua halafu pakua na chochote ukipendacho na ufurahie.

  • Tags

You can share this post!

Zifahamu baadhi ya faida za upupu (stinging nettle)

Wakenya 5 milioni wameathiriwa na njaa, ripoti yabainisha

T L