NA MWORIA MUCHINA
NYOKA anayeitwa ‘Vietnamese Long-Nosed Snake’, ambaye jina lake la kisayansi ni Gonyosoma boulengeri, ana pua iliyochomoka kama pembe ya kifaru.
Mfano huu wa pua ndio ulisababisha wanasayansi kumpa jina lingine la ‘rhinoceros ratsnake’.
Hata ingawa aina hii ya pua haina kazi ya ziada inafanya kwa nyoka hawa, wanasayansi wanaamini ilitokana na mabadiliko ya maumbile.
Nyoka hawa hula wanyama kama panya na wanapatikana kwenye misitu na nyika karibu na maeneo ya maji au mito.
Kadri wanavyozeeka nyoka hawa ndivyo wanabadilika rangi ya ngozi.