NA PAULINE ONGAJI
SHIDA ya uvimbe kujitokeza katika sehemu ya ndani ya pua la mtoto husababishia wazazi wengi wasiwasi.
Hali hii inayotambulika kama Nasal Polyps kwa lugha ya kitalamu, huhusisha kuvimba kwa njia ya pua na kwenye mianzi ya pua kwa zaidi ya wiki 12.
Uvimbe huu huwa mwepesi na hausabaishi maumivu, na hivyo ikiwa uvimbe ni mdogo sio rahisi kuutambua. Zikiwa nyingi au kubwa zaweza ziba mianzi ya pua.Mbali na watoto, hali hii pia huwakumba watu wenye umri wa makamo, lakini shida huisha baada ya matibabu. Hata hivyo, ni kawaida kwa uvimbe huu kujitokeza tena hata baada ya kutibiwa.?Ishara za uwepo kwa uvimbe puani
Kutokwa na kamasi kila mara Pua kuziba kwa muda mrefu Kukohoa na kukumbwa na matatizo unapomeza chakula Kutokuwa na hisia za kunusa au ladha Kuumwa na kichwa Uchungu kwenye meno Kukoroma unapolala Mwasho kwenye macho
Unatakiwa kumwona daktari ikiwa dalili hizi zitaendelea kwa zaidi ya siku kumi.
Kumbuka kuwa ishara hizi ni sawa na za mafua.
Aidha, unashauriwa kutafuta usaidizi wa kimatibabu endapo utashuhudia dalili zifuatazo:
Ni nini kinachosababisha hali hii? Ingawa kuna tafiti kadhaa kuhusu nasal polyps, wanasayansi hawajafanikiwa kupata sababu halisi zinazochochea hali hii.
Matibabu tofauti hutumika kutibu hali hii lakini hutegemea na kiwango cha uvimbe. Matibabu huangazia sana jinsi ya kupunguza saizi ya uvimbe ili kukabiliana na ishara.